Quantcast
Channel: Siasa Huru
Viewing all 2111 articles
Browse latest View live

Video : Rais Magufuli Alivyoongoza Wananchi Kuaga Mwili wa Dr Masaburi Dar

$
0
0
VIONGOZI MBALIMBALI WAMEJITOKEZA KUAGA MWILI WA DKT DIDAS MASABURI,VIWANJA VYA KARIMJEE JIJINI DAR LEO .
SANDUKU LENYE  MWILI WA MAREHEMU DKT DIDAS MASABURI LIKIWASILI VIWANJA VYA KARIMJEE,JIJINI DAR ES SALAAM ASUBUHI HII KWA AJILI YA KUTOLEWA HESHIMA ZA MWISHO,AMBAPO RAIS DKT JOHN POMBE MAGUFULI ALIWAONGOZA WANANCHI WALIOFIKA KUSHIRIKI KUAGA MWILI WA DKT DIDAS MASABURI.

Mwanamke Mwenye Wivu ni Mchunguzi Hatari

$
0
0
Ni usemi maarufu uliotungiwa kitabu na kuchezwa katika filamu, kuwa mwanamke mwenye wivu ni mpelelezi mzuri na mweledi kuliko polisi au afisa mpelelezi, hasa linapokuja suala la kufahamu mumewe, mpenzi wake anachepuka na nani?

Mwanamke mwenye wivu anaweza kupata taarifa zote za mpinzani wake ndani ya dakika tano tu.

Kengele ya hatari itakapogonga kichwani kuhusu mwizi wake, atamsaka katika mtandao wa Facebook, Instagram, Twitter na kupiga simu kwa watu anaowaamini...ndani ya dakika tano taarifa zote anazo mkononi.

Utakapomsikia mwanamke anakwambia nataka tuzungumze kuhusu fulani, jua taarifa zote anazo mkononi.

Utafiti

Kuna tafiti nyingi na ushuhuda unaodhihirisha hilo, huku katika jamii zetu kila kukicha tukishuhudia ugomvi, kelele, malumbano baada ya wanawake kufanikiwa kubaini walichokuwa wakikitafuta muda mrefu.

Utafiti uliofanywa na kampuni inayojihusisha na msaada ya sheria ya nchini Australia Slater & Gordon, unaonyesha namna ambavyo wanawake wanaweza kuwa wachunguzi wazuri kuliko polisi au shirika la upelelezi linapokuja suala la mapenzi.

Katika kisa kimojawapo kinacholibainisha hilo ni mwanamke anapoamua kupoteza muda mrefu kutafuta ukweli ili umuweke huru.

Mwanasheria wa familia wa kampuni iliyofanya utafiti huo Kaleel Anwar anasema wanawake sita kati ya 10 hutumia mitandao ya kijamii kufuatilia nyendo za waume zao. “Huunganisha matukio kwa kutizama ujumbe wanaotumiana kupitia mitandao ya kijamii. Wapo makini na upelelezi wao.”

Mchunguzi

Magdalena Luisou anasema aliwahi kubaini mumewe ana mpenzi wa nje kwa kuunganisha mawasiliano yao katika mtandao wa Facebook.

Anasema kila mumewe alipokuwa akichangia mada kwenye mtandao huo, mwanamke huyo alichangia.

“Niliingia kwenye ukurasa wake na kukuta miongoni mwa rafiki zake na wa karibu mume wangu yumo, kazi anayofanya ni tofauti na mume wangu, alikosoma pia ni tofauti, sikuona sababu iliyowafanya wawe karibu kiasi hicho nikatia shaka na kuazimia kufuatilia, ” anasema Luisou.

Hivyo akatafuta namba ya msaidizi wa mumewe wa ofisini na kumpigia mara kwa mara kwa ajili ya salamu kwa muda wa mwezi mmoja kabla ya kuanza kumpeleleza, kama miongoni mwa wageni wanaofika ofisini kumtembelea yupo wa wajihi kama wa huyo dada anayemuhisi.

Hakupata jibu la moja kwa moja zaidi ya kuendelea kuhisi hisi, “Nikamwambia mume wangu akitoka aniambie na ninapomuona yupo mtandaoni najua anachati na kumuuliza msaidizi wake kama yupo ofisini, siku ya kwanza alinijibu yupo na siku ya pili akasema ametoka muda siyo mrefu na baada ya muda akatoweka hewani, ”anasema.

Anasema kwa muunganiko huo na salamu alizoona wamepeana kwenye facebook asubuhi akafahamu watakuwa wote wamepumzika mahali.

Anasema alipompigia simu hakupokea, kwa kuwa alikuwa namba za yule dada nae alipompigia hakupokea.

Anafafanua kuwa aliamua kuweka kambi ya siri kwa kujificha karibu na ofisini kwa mumewe kwa kukaa sehemu iliyomuwezesha kuona kila anayeingia na kutoka, japo ilikuwa taabu kidogo kutokana na kuwa na watu wengi.

“Siku moja kwa mshangao mkubwa taksi ilisimama na aliyeshuka alikuwa ni yule dada anayemuhisi akiwa na begi na kukaa nje kwa muda kabla ya mumewe kutoka na wote kuingia kwenye gari ya mumewe na kuondoka, ”anasema.

Hawawezi kuwaacha

Utafiti huo wa Slater & Gordon umeonyesha zaidi ya asilimia moja kwa kila wanawake sita wanasema hawawezi kuwaacha waume zao hata wakigundua wanawasaliti kimapenzi.

Pia umeonyesha kuna tofauti ya kuaminiana kati ya wanawake na wanaume ambapo asilimia 36 ya wanawake na asilimia 24 ya wanaume wanadhani wapenzi wao sio waaminifu, huku asilimia moja kati ya sita huangalia historia za wapenzi wao ikiwamo katika simu, kompyuta.

Umeonyesha pia asilimia 10 ya wanawake hupiga simu ofisini kwa wame zao kuwauliza wasaidizi wao kama kweli wapo kazini.

Asilimia 30 wanakiri kuwa licha ya kuwafuatilia wame zao kwa muda mrefu hawajabahatika kuwafuma, huku asilimia 70 wakisema kuwa hawajawahi kukosea kuwafuma ikiwa ni pamoja na wanapokuwa wametoka kwa ajili ya chakula, semina, hotelini kwa ajili ya mapumziko.

Halima Yahaya anasema siyo kazi ngumu kugundua tabia mpya za mumewe kutokana na kumfuatilia.

Anasema akirudi kazini kwa kumtizama na kusikia sauti yake hugundua kama ana tatizo na akifanya nae mahojiano machache hugundua kama ni la kiofisi au binafsi, ingawa huwa ngumu kugundua kama ni binafsi ni lipi hasa.

“Kwa kuwa kila siku nahisi naibiwa mara nyingi huwa nafikiria fikiria ameudhiwa na mwanamke ndiyo maana amerudi muda huo, ”anasema.

Anafafanua kutokana na tabia hiyo hata anapokuwa na uhusiano wa nje huwa rahisi kubaini hivyo huanza kufuatilia, ikiwamo alimbaini mumewe kwa njia hiyo.

“Tulikuwa tunakula wote chakula cha jioni, ghafla akaanza kukataa na kusema atakula baadae”

“Hilo lilinistua na kuanza kufuatilia kwa nini amebadili tabia ghafla” anasema.

Anasema aliendelea kufuatilia na alipokuwa akiingia ndani kulala hafungi mlango vizuri anasikiliza nini kinaendelea sebuleni kwa sababu hawakuwa wengi alikuwa mtoto wao mmoja, msichana wa kazi na binamu yake aliyekuja kuwatembelea siku siyo nyingi.

Anafafanua hali ya nyumba hiyo kuwa vyumba vyote vina milango kasoro cha wageni ambacho ndiyo alikuwa analala binamu yake.

“Siku kama mbili hivi za kufuatilia nyendo zake nilibaini akinyata minyato yake huishi korido nikawa najiuliza inaishia wapi, nikaanza kufuatilia na kubaini inakosihia.

“Nilisubiri ajisahau sebuleni, nikaingia kwenye chumba anacholala binamu yangu na kumnyamazisha kwa ishara ya kuweka kidole mdomoni na baada ya dakika 45 uchunguzi wangu ulitimia kwa sababu mume wangu waliingia na kujilaza pembeni ya binamu yangu bila kujua kama nipo, nikawasha taa na kumuumbua, ”anasema Yahaya.

Yahaya anasema kwa ushahidi huo hakuwa na jinsi ya kukataa, lakini angemuuliza asingekubali.

Mwanasaikolojia wa kampuni iliyofanya utafiti Bilgram Johnson anasema wanawake kwa kawaida wana uwezo zaidi wa kubaini mabadiliko ya wenza wao ukilinganisha na wanaume.

Anasema utafiti huo ulibaini mwanamke ni ngumu kushtukiwa kama ameanza uhusiano sehemu na anapoulizwa swali lolote hujiuliza kwa nini kaulizwa hivyo kabla ya kujibu , ukilinganisha na wanaume ambao hujibu haraka na kuwarahisishia wanawake upelelezi wao.

Utafiti huo uliohusisha madaktari wa afya, wataalamu wa saikolojia, wanasheria , ulibaini kuwa asilimia tano wanafahamu kumpeleleza mtu kwa siri ni kuingilia haki yake ya msingi, asilimia 17 walisema kufanya hivyo kunawapa amani ya nafsi na akili kuliko kuendelea kuhisi.

 By Kalunde Jamal

Wafanyakazi TBS, TRA Wakalia Kuti Kavu

$
0
0
Serikali imewataka baadhi ya wafanyakazi wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS) walioshirikiana na wenzao wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kupitisha  makontena zaidi ya 100 bila kukaguliwa na shirika hilo katika Bandari ya Dar es Salaam kujisalimisha haraka.

Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage alitoa agizo hilo jana wakati akizindua baraza la wafanyakazi wa TBS.

“Nimeanza kukusanya orodha ya majina ya watu waliosaidia kupitisha makontena haya na nikija nayo hawatapona,” alisema.

Aliwataka wote wanaojijua kuhusika kujisalimisha mapema na kutubu ili wasamehewe kabla ya hatua hiyo.

Makontena hayo yalipitishwa katika Bandari ya Dar es Salaam hivi karibuni bila ya kuthibitishwa na TBS.

Pia, aliitaka TRA kuacha kutoa makontena bila ya shirika hilo kuthibitisha au kukagua ubora wa bidhaa zinazoingizwa nchini kwa sababu ndilo lenye mamlaka hayo.

Alisema watakaotubu watapaswa kusema walishiriki vipi na lini, walishirikiana na nani na kutaja sehemu yalikopelekwa ili Serikali iweze kusaidia kukomesha hali hiyo.

Mwijage alisema anaamini waliofanya hivyo katika mamlaka hiyo walifanya kwa utashi wao bila ya ushiriki wa viongozi wao na kwamba sasa wakati umefika wa kukomesha tabia hiyo.

Alilitaka baraza hilo jipya la wafanyakazi kushirikiana na menejimenti kuhakikisha matatizo yanayojitokeza yanapatiwa ufumbuzi kwa masilahi ya nchi na kwamba Serikali itahakikisha inaongeza vitendea kazi na watumishi ili kufikia malengo ya shirika.

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TBS, Dk Egid Mubofu alisema baraza hilo lina wajumbe 48 wanaotoka katika vitengo mbalimbali na litakaa kwa muda wa miaka mitano.

“Baraza hili linaundwa kutokana na mkataba wa menejimenti na Chama cha Wafanyakazi (Raawu),” alisema Dk Mubofu.

Alisema wafanyakazi wanatakiwa kufanya kazi kwa weledi na uadilifu katika majukumu yao ya kila siku.

Mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi TBS, Profesa Mekanya Maboko alilitaka baraza hilo kufanya kazi kwa kushirikiana na menejimenti na bodi kuhakikisha shughuli za udhibiti wa ubora zinafanyika kwa ufanisi.

“Bodi itaendelea kuisimamia menejimenti na kuishauri ifanye kazi kwa kuzingatia sera na sheria,” alisema.

Pogba Afunguka Kwa Mara ya Kwanza Juu ya Kiwango Chake Kibovu Ndani ya Man United

$
0
0
Mchezaji wa Manchester United, Paul Pogba amefunguka kwa mara ya kwanza juu ya lawama anazotupiwa kwa kiwango chake kibovu anachokionyesha klabuni hapo tangu asajiliwe msimu huu kwa kiasi cha paundi milioni 89 kilichoweka rekodi ya dunia.

Pogba ameiambia French TV kuwa anahitaji muda ili aweze kuzoea mazingira ya uchezaji ndani ya timu hiyo.

“I will need a little time to adapt in Manchester, time for the machine to start working. I am adapting, People like to talk about Paul Pogba. The critics, they stay for a day, then after that I put my music back on, I dance,” amesema Pogba.

Mpaka sasa Man United inashika nafasi ya saba kwenye ligi kuu ya Uingereza huku usiku wa Jumatatu hii timu hiyo itakuwa ugenini kwenye uwanja wa Anfield kucheza na Liverpool kwenye muendelezo wa ligi kuu ya nchini hiyo.

Lizer wa ‘Wasafi Records’ Aeleza Changamoto Aliyopata Baada ya Kuaanza Kufanya Kazi na Wasanii wa ‘WCB’

$
0
0
Mtayarishaji wa muziki kutoka ‘Wasafi Record’, Lizer amefunguka kwa kusema kuwa aina ya muziki anaofanya haikupendwa na viongozi wa label hiyo.

Lizer ambaye tayari ameshafanya hits kadhaa za wasanii wa WCB, amesema aliwalazimisha kuukubali muziki wake ili kuwa tofauti na maproducer hapa.

“Changamoto ambayo nilikutana nayo kwanza nilileta muziki mwingine ambao ulikuwa tofauti na wao walikuwa na muziki wao,” Lizer aliiambia FNL ya EATV. “Kwa hiyo walikuwa wanajaribu kuni-force niwe kama producer wa hapa, lakini mimi nikasema nikiwa kama producer wa hapa nitakuwa sijaleta kitu kipya natakiwa kuwa tofauti kidogo. Kwa hiyo niliwalazimisha muziki wangu na nashukuru mungu watu wameupokea vizuri na wao tunaenda sawa,”

Pia Lizer alisema siyo kweli kwamba Harmonize anamwiga Diamond kuimba ambapo amedai wasanii hao kila mmoja ana muziki wake.

Stori Mpya Kuhusu Sababu ya Scorpion Kumtoboa Mtu Macho

$
0
0
Makala hii imeanza kuzunguka katika mitandao mbalimbali ya kijamii leo asubuhi ikielezwa kutoka kwa mkazi wa Buguruni anayesema anakifahamu vyema kisa cha Scorpion kumtoaboa macho mkazi wa Dar es Salaam aliyefahamika kwa jina la Said Ally.

Katika habari zilizotolewa na mhanga, alisema kuwa alikuwa akitokea kazini kuelekea nyumbani na alipokuwa akinunua mahitaji yake ya nyumbani eneo la Buguruni, ndipo alivamiwa na mtu huyu anayefahamika kama Scorpion na kumfanyia ukatili huo.

Hii hapa chini ndiyo stori mpya inayoeleza kwa upande mwingine sababu za tukio hilo.

Inaelekea wanaume wa mkoani hawamjui scorpion. Halafu sisi watu wa Buguruni tunamjua huyo Saidi na shughuli zake, na pia tunajua shighuli za Scorpion ndio maana watu hata hawakuhangaika nao.

Watu waliwaacha wamalize mambo yao.

Tunaangalia tu watu wanavyo shadadia mambo wasiyoyajua kwa undani wakipiga kelele dunia nzima ikiwa ni pamoja na mkuu wa kaya ya Jiji.

Scorpion ni mtu aliyeamua kujichukulia sheria mkononi kwa kuwa uwezo huo anao.
Kwa maana ya uwezo wa kupambana na mtu yoyote ambae ni mtukutu. Anapiga kareti kama za kwenye kideo na physic yake sio ya wanaume hata 2 wa kawaida. He is a man na nyongeza.

Kwa kifupi ni kwamba Buguruni kuna watu watanashati na wanashughuli zao za maana lakini wanamiliki mitandao ya vibaka ambao hupora na kuwaletea mizigo wanayopora.

Na hiyo ndio wanapopatia hela zao nyingi.

Hujawahi kujiuliza Tv, radio, vipochi, simu na vitu vingine kama hivyo vikiibiwa huwa vinaenda wapi?

Wale waibaji huenda na kumkabidhi mtu halafu wanapewa hela flani ndogo(ya kula).
Yeye huvitakatisha vile vitu kwa kuviuza kupitia legitimate channels kwa yeye hubaki kuwa mtu legit.

Scorpion alikua ametangaza kiama kwa vibaka pale Buguruni. Na alikua anawashughulikia kweli. Hivyo he was posing a danger kwenye biashara za watu.
Wakati vibaka wakindelea kushughulikiwa na hali ikionekana imeanza kuwa swari, yani vibaki waliosalia wanahamia kambi nyingine kama vingunguti, gomz etc.
Ndugu wa kike wa mpiga kareti (rafiki wa scorpion) akaporwa pochi iliyokua na simu maeneo ya Buguruni sheli.

Scorpion akaamua kumsaka muhusika na hakufanikiwa kumtambua. Akaamua kutuma ujumbe kwa mkuu wao ambae ndie mhanga wa macho, kuwa anataka arejeshewe mali iliyoporwa.

Kama kawaida ya wapanga misheni mkuu akapiga kimya.

So Scorpion akaamua kudeal nae, the boss himself ndio akamfuata alipomkuta and the rest of the story baada ya kumfuata face to face mtakua mmeipata kwenye media.

Sasa nyie mpeni mamilioni na assets bosi wa wahalifu kisa mnamhurumia wakati hamumjui.

Ndio maana watu hawakutaka kuingilia kesi wakati jamaa anasurubiwa. Sie wa buguruni tunaelewa.

Mtu hakurupuki tu kumtoboa toboa mtu asiyemjua.

Masaburi Atajwa Kama Mtu aliyelifanya jiji la Dar kuwa Maarufu Duniani

$
0
0
Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, Isaya Mwita leo amekiri kuwa mtangulizi wake ambaye amefariki dunia, Didas Masaburi alifanya kazi kubwa ya kuboresha miundombinu ya jiji hilo pamoja na kulitambulisha katika anga za kimataifa.

Meya Mwita ameyasema hayo leo Jijini Dar es Salaam katika safari ya mwisho ya kuuaga mwili wa Marehemu Masaburi aliyefariki dunia usiku wa kuamkia Alhamisi katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.

“Binadamu anapokuwa ameondoka huwa tunazungumza mema aliyoyafanya katika jamii yetu. Mimi Sikuwahi kufanya nae kazi lakini nimekuta kazi ambazo amefanya katika halmashauri ya jiji,” amesema.

Ameongeza kuwa “Moja ya mambo ambayo sitasahau niliyoyakuta aliyoyafanya katika utawala wake ni kuuleta mradi wa DMDP uliolenga kusukuma na kutaka kuboresha maeneo ya miundombinu ya DSM, ukiona kazi aliyoacha mimi ndio naendelea nayo sasa.”

Amesema jambo lingine alilofanya Marehemu Masaburi enzi za utawala wake ni kuleta miji mikubwa duniani kuja kuwekeza na kutoa misaada ya kimaendeleo nchini.

Miongoni mwa majiji aliyoyataja Mwita ni jiji la Hamburg, Shanghai na Torotonto.

“Aliileta hapa miji mikubwa duniani, mimi napata mialiko sasa katika nchi mbalimbali na hii ni matunda ya jitihada zake katika kulitangaza jiji la Dar es Salaam na Tanzania kwa ujumla.” amesema.

Pia Meya Mwita amesema kuwa, Masaburi alifanikiwa kutoa mamlaka na madaraka ya kiutendaji kutoka serikali kuu hadi serikali za mitaa.

“Alipokuwa akiongolea dhana kubwa ya kutoa madaraka kutoka serikali kuu kuja serikali za mitaahili, alikuwa anamaanisha. Jambo hili si jepesi kwa kuwa, halmashauri za mitaa bila ya kuwa na nguvu kubwa haziwezi leta maendeleo mfano Kenya na Uganda halmashauri zake zinauwezo na mamlaka ya kupanga maendeleo,” amesema.

Amesisitiza kuwa “Japo hakufanikiwa kwa kiwango hicho mawazo yake yataishi na mimi kama mrithi wake nitaendelea kuyaenzi.”

Marehemu Didas Masaburi enzi za uhai wake aliwahi kuwa Diwani wa Kata ya Kivukoni, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Tawala za Serikali za Mitaa (ALAT).

ATCL Yatoa Ofa Ya Mwezi Mmoja Kwa Safari Za Mwanza.

$
0
0
Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL) imetoa ofa ya mwezi mmoja kwa abira wanaosafiri kutoka Dar es salaam kwenda Mwanza kulipa nauli ya shilingi 160,000/- kwa safari moja.

Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dar es salaam na na Kaimu Afisa Mawasiliano wa Kampuni Bi.Lily Fungamtama wakati akiongea na Idara ya Habari.

Amesema Ndege za Kampuni zimeanza kutoa huduma kuanzia Jumamosi ya wiki iliyopita ya tarehe 15 ya mwezi huu kama ilivyobainisha kupitia vyombo vya Habari.

Safari hizo zilianza kwa kutoa huduma ya kusafirisha abiria kuelekea nchini Comoro na hapa nchini itoa safari katika mikoa ya Mwanza, Arusha na Kigoma.

Bi.Fungamtama amesema kwa kuanzia walianza na mazoezi ya vitendo kwa marubani na wafanyakazi wa ndani ya Ndege ambapo hatimaye walianza safari za biashara ya kusafirisha abiria mnamo tarehe 15 Oktoba kama ilivyopangwa.

Ameongeza kuwa ATCL imeboresha huduma zake kwa kiasi kikubwa kwa kuwapatia wateja wake ofa ya kubeba kilo 20 za mizigo na kilo 7 za mzigo wa mkononi bure   pamoja na kutoa vinywaji na ubadilishaji wa tiketi ni bure ndani ya mwezi.

Aidha, Kaimu Afisa Mawasiliano wa Kampuni Bi.Lily amekanusha taarifa potofu kuwa zimekwama kuanza safari zilizopangwa.

Amesema kuwa habari hizo sio za kweli kwani hivi sasa wameshaanza huduma katika mikoa hiyo mitatu.

Kampuni ya Ndege ya ATCL kwa sasa ina ndege tatu,zikiwemo mbili aina ya Dash8-Q400 zenye uwezo wa kubeba abiria 76 kila moja na Dash8-Q300 moja yenye uwezo wa kubeba  abiria 50.

Dully Sykes Ataja Sababu ya Kumkubali zaidi Diamond Kuliko Wasanii Wengine

$
0
0
Msanii mkongwe wa muziki wa Bongo Fleva, Dully Sykes amefunguka sababu ya kumkubali zaidi Diamond Platnumz kuliko wasanii wengine.


Muimbaji huyo ameiambia Times FM kuwa anamkubali zaidi Diamond kwakuwa amekuwa akimheshimu zaidi.

“Watu wanalalamikaga ‘oooh’ namsifia sana Diamond, nisiongee uongo nakubali wote wananiheshimu lakini Diamond ananiheshimu na kunionesha nidhamu zaidi,” amesema Dully.

Dully ameongeza kuwa kuna kipindi Diamond aliwahi kuinama mbele za watu na kumfunga kamba zake za viatu zilizokuwa zinafunguka.

Wasioamini uwepo wa Mungu Kenya wataka kuondolewa neno ‘God’ kwenye wimbo wa taifa

$
0
0
Chama cha watu wasioamini uwepo wa Mungu (Atheists) nchini Kenya kimetaka kuondolewa kwa neno ‘God’ kwenye wimbo wa taifa.

Wanadai kuwa neno ‘God” kwenye mstari wa kwanza wa wimbo huo halihimizi moyo wa umoja kwakuwa si Wakenya wote wanaomuamini Mungu.

Wamedai kuwa Kenya ni nchi isiyo na dini na hivyo kuimba wimbo wa taifa wenye neno ‘God’ inakinzana na katiba ya nchi hiyo. Wimbo wa taifa wa Kenya huanza na kwa kusema “Oh, God of all creation.”

Watu hao wamesema kuwa huhisi kutengwa kila wimbo huo unapoimbwa. Wamesema watapeleka malalamiko yao bungeni.

Maamuzi ya Umoja wa Ulaya Baada ya Burundi kujitoa Mahakama ya ICC

$
0
0
Siku chache baada ya Burundi kutangaza maamuzi ya kujitoa kwenye Mahakama ya makosa ya uhalifu ICC, Umoja wa Ulaya umetangaza kuitenga serikali ya Burundi kwenye masuala ya fedha za kikosi chake kilichotumwa nchini Somalia kujiunga na kikosi cha Umoja wa Afrika kusimamia amani nchini humo (AMISOM).

Umoja wa Ulaya, ambaye ni mfadhili mkuu wa Burundi unachangia 20% ya bajeti ya taifa hilo, umeamua kuchukua vikwazo dhidi ya serikali ya Burundi, inayotuhumiwa kwa ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu na kukataa mpaka sasa kuketi kwenye meza ya mazungumzo na upinzani wake.

Serikali ya Burundi imeendelea kutengwa katika ngazi za kimataifa, na kutuhumiwa uhalifu mbaya dhidi ya binadamu, Umoja wa Ulaya unataka kuzuia moja ya sehemu kuu zinazoipatia serikali ya Burundi fedha za kigeni.

Umoja wa Ulaya umechukua uamuzi wa kutopitisha tena mishahara ya askari wa nchi hiyo wanaosimamia amani nchini Somalia kwenye akaunti ya serikali.

Uamuzi wa EU unakuja wakati ambao uchumi wa Burundi umeendelea kudorora, hata baadhi ya shughuli zinazoingiza mapato kwa serikali zimekwama kutokana na hali mbaya ya kiuchumi

Ni wiki tatu sasa tangu Umoja wa Ulaya kutuma fedha kwenye akaunti ya Umoja wa Afrika ili kulipa mishahara askari wa kikosi cha Umoja wa Afrika nchini Somalia (AMISOM).

Ripoti kutoka Brussels Ubelgiji zinasema Umoja wa Ulaya umelipa tu malimbikizo ya kipindi kinachoishia hadi Machi 16, 2016, tarehe ambayo Umoja wa Ulaya uliiwekea vikwazo serikali ya Burundi, kwa mujibu wa Ibara ya 96 ya Mkataba wa Cotonou.

Tangu wakati huo, Umoja wa Ulaya ulisimamisha misaada yake ya moja kwa moja kwa serikal ya Burundi. Ni Euro milioni 5 tu za mishahara ya askari 5,500 wa Burundi wa kikosi cha AMISOM zimekua zikipitishwa kwenye hazina ya serikali ya Burundi.

Nicki Minaj Ampa za Uso Donald Trump na Mkewe Melania

$
0
0
Mastaa wa Marekani wameendelea kumuandama mgombea wa Urais wa Marekani kupitia chama cha Republican, Donald Trump – sasa ni zamu ya Nicki Minaj.

Kwenye tamasha la Tidal X 1015 lililofanyika wikiendi hii huko mjini New York, rapper Nicki Minaj alimponda mgombea huyo anayechukiwa na watu wengi kwa vitendo vyake vya udhalilishaji kwa wanawake pamoja na sera zake za kuwapinga watu weusi.

“Barack needed Michelle, bitch, and Bill needed a motherf-cking Hillary. You better pray to God you don’t get stuck with a motherf-cking Melania,” amesema Nicki wakati wa tamasha hilo.

Mpaka sasa mastaa kadhaa wameonekana kumpinga mgombea huyo akiwemo Jon Stewart, Barbra Streisand, Samuel L. Jackson, Chelsea Handler, Lena Dunham na wengine.

Wanafunzi UDSM Walalamikia Vigezo Vipya Vya Utoaji wa Mikopo

$
0
0
Baadhi ya wanafunzi wanaosoma chuo kikuu cha Dar es salaam wameilalamikia serikali kupitia wizara ya Elimu kubadili vigezo vya utoaji wa mikopo bila taarifa jambo lililowasababishia usumbufu mkubwa wanafunzi waliofika chuoni hapo huku wakikabiliwa na maisha magumu baada ya kukosa fedha za kujikimu pamoja na malazi.

Mwisho mwa wiki wizara ya elimu ilitangaza majina ya wanafunzi watakaopata mikopo pamoja na vigezo vilivyotumika ikiwemo wanafunzi waliosoma masomo ya sayansi, wenye ufaulu wa juu na walemavu na yatima pamoja na ufaulu wa waombaji katika ameneo ya vipaumbele na umahiri huku vigezo hivyo vikiwaacha nje asilimia kubwa ya wanafunzi ambao wanachukua masomo sanaa.
Wakizungumzia adha hiyo wanafunzi hao wamesema hakuna aliyetarajia kutokea kwa hali hiyo kwani hawakutangaziwa mapema kwamba utaratibu wa utoaji wa mikopo umebadilika hivyo wazazi nao wazazi wamewasafirisha watoto wao kutoka mikoani wakitegemea udhamini kutoka bodi ya mikopo ambayo hata hivyo haijulikani ni lini itatolewa huku wakilandalanda mitaani bil kufahamu hatma yao.

Charles Kayoka ni mhadhiri wa chuo kikuu cha Dar es salaam ambaye anazungumzia mabadiliko hayo kuwa kutokuwepo kwa sera ya ya elimu ya kudumu ni moja ya sababu ambazo zinaifanya serikali kubadilisha taratibu zake kulingana na nyakati lakini pia ameikumbusha serikali kuwa haitaweza kufanikiwa katika utelekezaji wa kauli mbiu ya tanzania ya viwanda bila ya kuwepo na wataalamu waliosomea sanaa

Drogba Akataa Kuichezea Timu yake Baada ya Kuwekwa Benchi

$
0
0
Aliyekuwa mchezaji wa Chelsea Didier Drogba alikataa kuichezea Montreal Impact baada ya kuambiwa hataanzishwa dhidi ya Toronto ,kulingana na kocha Mauro Biello.

Drogba mwenye umri wa miaka 38 hakuwepo katika uwanja wa michezo wa Saputo ambapo Impact ilipata sare ya 2-2 na hivyobasi kuweza kufuzu kwa michuano ya muondoano ya ligi ya Marekani.

Montreal hapo awali ilikuwa imesema kuwa Drogba alikuwa anauguza jeraha la mgongo na hivyobasi asingeweza kucheza.

Lakini Biello alisema: Hakukubali kwamba angechezeshwa kama mchezaji wa ziada na mwishowe hakutaka kushirikishwa katika kikosi cha watu 18.

Kocha huyo aliongezea: Alikuwa na tatizo katika mgongo wake lakini alikuwa anaweza kucheza.

Drogba ambaye aliondoka Chelsea mwezi Julai 2015 amekuwa akitumiwa kama mchezaji wa ziada katika mechi mbili kati ya nne.

Amefunga mabao 10 katika mechi 21 msimu huu.

Jakaya na Edward Lowassa Ana Kwa Ana Msibani Dar

$
0
0
Jakaya Kikwete na Edward Lowassa walikuwa marafiki na sasa ni maadui wakubwa wa kisiasa, lakini jana walilazimika kushikana mikono wakati wa ibada ya kuaga mwili wa kada wa CCM, Didas Masaburi.

Mbali na tukio hilo, Rais John Magufuli alituliza wafiwa alipoeleza kuwa Masaburi, ambaye alizikwa jana chuoni kwake Chanika Dar es Salaam, ameacha wake wapatao watano na watoto zaidi ya 20 baada ya minong’ono kuibuka kutokana na aliyesoma wasifu kusema kada huyo ameacha mke mmoja wa ndoa na wajane wawili.


Mbunge Apokea Mishahara Mitano ya Utumishi Hewa

$
0
0
Sakata la watumishi hewa sasa limefikia pabaya baada ya msako wa watu wanaolipwa fedha bila kuwapo kazini kumkumba Mbunge Makete (CCM), Profesa Norman Sigalla ambaye alikuwa mkuu wa Wilaya ya Songea.

Wadau walishawahi kueleza kuwa msako wa watumishi hewa uliwahusu wafanyakazi wa kariba ya chini na hivyo kuokoa fedha kidogo, lakini sakata la Profesa Sigalla limeonyesha kuwa hata kariba ya juu serikalini inahusika.

Profesa Sigalla anadaiwa kupokea mshahara wa ukuu wa wilaya kwa miezi mitano baada ya kuacha kazi hiyo wakati wa Uchaguzi Mkuu na baadaye kuchaguliwa kuwa mbunge kwa tiketi ya CCM.

Hali hiyo imeisababishia Serikali hasara ya Sh23 milioni.

Baada ya kuacha kazi hiyo ya kuteuliwa na Rais, inadaiwa kuwa Profesa Sigalla aliendelea kupokea mshahara wake wa ukuu wa wilaya wa Sh4.6 milioni kutokana na ofisa utumishi wa ofisi ya katibu tawala wa Mkoa wa Ruvuma kumrudisha kwenye orodha ya malipo ya mshahara.


Wadau wa Elimu Wamgeuzia Kibao Joseph Mungai

$
0
0
Siku moja baada ya aliyekuwa Waziri wa Elimu katika Awamu ya Tatu, Joseph Mungai kusema hakuvuruga mfumo wa elimu katika uongozi wake, wadau wa sekta hiyo wamepinga wakisema  umevurugwa na mawaziri kwa kutofuata Sheria ya Elimu ya mwaka 1979 na kujiamulia mambo.

Mungai ambaye alikuwa akijibu tuhuma zilizoelekezwa kwake baada ya kustaafu siasa alisema Rais wa Awamu ya Nne, Jakaya Kikwete hakumteua kuendelea kuongoza elimu kwa kuwa alitaka kufurahisha walimu waliokuwa wakimchukia kutokana na kuwabana.

Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT), Ezekiah Oluochi alisema mawaziri waliopita na aliyepo sasa wamenchangia kushuka kwa kiwango cha elimu kwa asilimia 90 kwa kutofuata sheria ya elimu.


Mauzo ya Hisa Katika Soko la Hisa Dar (DSE) Yaporomoka Kwa Asilimia 94

$
0
0
Mauzo ya Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE) yameshuka katika kipindi cha wiki iliyopita kwa 91% kutoka Tsh 32.5 Bilioni na kufikia Tsh 3 Billion. Pia Idadi ya hisa zilizouzwa na kununuliwa zimeshuka kwa 94% kutoka 9 millioni hadi laki 5.

Afisa Masoko Mwandamizi wa DSE, Marry Kinabo, wakati akisungumza na waandishi wa habari jana, alisema kilichochangia kushuka kwa idadi ya mauzo ya hisa ni kutokana na wiki husika kuwa na siku pungufu za kazi na kwamba mauzo ya hisa hizo yalifanyika kuanzia Jumatatu hadi Alhamisi ya tarehe 13 ambapo siku iliyofuata (Ijumaa) ilikuwa siku kuu ya kumbukumbu ya Kifo cha Baba wa Taifa Mwl. Julias Kambarage Nyerere.

Vile vile, Kinabo alisema kuwa, kutokana na idadi ya mauzo ya hisa kushuka, kumepelekea ukubwa wa mtaji wa soko hilo kushuka kwa 3% kutoka Trilioni 21.49 hadi Trilioni 20.8

Aidha, alitaja kampuni zinazoongoza kwa idadi ya hisa zilizouzwa na kununuliwa kuwa ni CRDB kwa 53%, TCC 41% na TBL 4%.

Hata hivyo, alisema mtaji wa makampuni ya ndani umebaki kwenye kiwango kile kile cha Trilioni 8.13 wakati viashiria katika Sekta ya viwanda (IA), Sekta ya huduma za kibenki na kifedha (BI) na Sekta ya huduma za kibiashara (CS) wiki hii umebaki kama awali.

Wajeruhiwa kwa Bomu Wakimkamata Mtuhumiwa

$
0
0
Polisi na raia wanne wamejeruhiwa kwa bomu la kutupwa kwa mkono walipokuwa wakimkamata mtuhumiwa wa ujambazi kwenye Kijiji cha Uvinza mkoani Kigoma.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kigoma, Ferdinand Mtui alisema jana kuwa tukio hilo lilitokea Oktoba 14.

Mtui aliwataja majeruhi hao kuwa ni askari polisi F.3187 Koplo Isaya na raia Saidi Mohamed, Seleman Kashali, Joseph Daudi na Hassan Nasibu, wote wakazi wa Kijiji cha Uvinza.

Msanii Roma Afunguka Kuhusu Mtoto wake wa Nje ya Ndoa

$
0
0
Msanii Roma Mkatoliki amempa zawadi ya wimbo mtoto wake anayeitwa Ivan katika siku yake ya kuzaliwa ambapo ametimiza miaka minne, lakini kuna tetesi kuwa rapa huyo ana mtoto mwingine nje ya ndoa.

Ukiongelea wasanii ambao wanafanya vizuri kwa upande wa hip hop huwezi kuacha jina la Roma Mkatoliki.

eNewz ilipiga story na Roma na alisema kuwa hizo skendo hazikuanza leo kwa sababu tayari aliwahi kupata skendo ya yeye na aliyekuwa mtangazaji wa kipind cha TV cha Nirvana, Lotus Kyamba kuwa mtoto aliyenaye ni wa kwake licha ya kwamba siyo kweli na kwamba yeye ana mtoto mmaja pekee ambaye ni Ivan

“Mimi kiukweli nina mtoto mmoja tu wa kiume ambaye ni Ivan na hizo story za mimi kuwa na mtoto nje zipo niliwahi kuambiwa nina mtoto na lotus kumbe siyo kweli na huwa sipendi kuziongelea sana kwa sababu mimi nina mke wangu na nina mtoto mmoja tu ambaye ni Ivan”
Viewing all 2111 articles
Browse latest View live